1 Mfalme Sulemani akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini[a], upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi[b]. 2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini[c] ingeweza kuizunguka. 3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja[d]. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini, na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana. 5 Unene wake ulikuwa nyanda moja[e], na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Ingejazwa na bathi elfu tatu[f].
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ya makuhani kunawia.
7 Akatengeneza vinara kumi vya taa vya dhahabu kama ilivyoainishwa na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini, na vitano upande wa kaskazini.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli mia moja ya dhahabu ya kunyunyizia.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani, na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba. 10 Akaiweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini-mashariki mwa nyumba.
11 Huramu pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia.
19 Sulemani pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu:
Languages