Link to home pageLanguagesLink to all Bible versions on this site
Zaburi 150
Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake
1 Msifuni Bwana.
 
Msifuni Mungu katika patakatifu pake,
msifuni katika mbingu zake kuu.
2 Msifuni kwa matendo yake makuu,
msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,
msifuni kwa kinubi na zeze,
4 msifuni kwa matari na kucheza,
msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5 msifuni kwa matoazi yaliayo,
msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
 
6 Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana.
 
Msifuni Bwana!

<- Zaburi 149
  • Zaburi