Link to home pageLanguagesLink to all Bible versions on this site
Zaburi 14
Uovu Wa Wanadamu
(Zaburi 53)
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.
 
2 Bwana anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 Wote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!
 
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Bwana?
5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,
bali Bwana ndiye kimbilio lao.
 
7 Laiti wokovu wa Israeli
ungalikuja kutoka Sayuni!
Wakati Bwana arejeshapo
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!

<- Zaburi 13Zaburi 15 ->
  • Zaburi