Link to home pageLanguagesLink to all Bible versions on this site
Zaburi 134
Wito Wa Kumsifu Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
1 Msifuni Bwana, ninyi nyote watumishi wa Bwana,
ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Bwana.
2 Inueni mikono yenu katika pale patakatifu
na kumsifu Bwana.
 
3 Naye Bwana, Muumba wa mbingu na dunia,
awabariki kutoka Sayuni.

<- Zaburi 133Zaburi 135 ->
  • Zaburi