Link to home pageLanguagesLink to all Bible versions on this site
25
Bildadi Anasema: Mwanadamu Awezaje Kuwa Mwadilifu Mbele Za Mungu?

1 Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:

2 “Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3 Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4 Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5 Ikiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
6 sembuse mtu ambaye ni funza:
mwanadamu ambaye ni buu tu!”

<- Ayubu 24Ayubu 26 ->